Skip to content
1 Wathesalonike 4:7

1 Wathesalonike 4:7

Inaonyesha mstari 7 pamoja na muktadha unaouzunguka.
4
ili kwamba kila mmoja wenu ajifunze kuutawala mwili wake mwenyewe katika utakatifu na heshima,
5
si kwa tamaa mbaya kama watu wa Mataifa wasiomjua Mungu.
6
Katika jambo hili mtu asimkosee ndugu yake wala kumlaghai. Kwa kuwa Bwana ni mlipiza kisasi katika mambo haya yote, kama vile tulivyokwisha kuwaambia mapema na kuwaonya vikali.
7
Kwa maana Mungu hakutuitia uchafu, bali utakatifu.
8
Kwa hiyo, mtu yeyote anayekataa mafundisho haya hamkatai mwanadamu, bali anamkataa Mungu anayewapa ninyi Roho wake Mtakatifu.
9
Sasa kuhusu upendo wa ndugu hamna haja mtu yeyote kuwaandikia, kwa maana ninyi wenyewe mmefundishwa na Mungu kupendana.
10
Nanyi kwa kweli mnawapenda ndugu wote katika Makedonia nzima. Lakini ndugu, tunawasihi mzidi sana kuwapenda.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options