Skip to content
1 Nyakati 12:1-7

1 Nyakati 12:1-7

1
Hawa ndio watu waliomjia Daudi huko Siklagi, wakati alikuwa amefukuzwa mbele ya Sauli mwana wa Kishi (walikuwa miongoni mwa mashujaa waliomsaidia Daudi vitani,
2
walikuwa na pinde na walikuwa na uwezo wa kupiga mishale au kutupa mawe kwa kombeo wakitumia mkono wa kushoto au wa kulia; hawa walikuwa ndugu zake Sauli kutoka kabila la Benyamini):
3
Mkuu wao alikuwa Ahiezeri, na wa pili Yoashi, wote wana wa Shemaa Mgibeathi; pia Yezieli na Peleti wana wa Azmawethi; Beraka, Yehu Mwanathothi,
4
na Ishmaya Mgibeoni, shujaa miongoni mwa wale Thelathini, ambaye alikuwa kiongozi wa wale Thelathini; Yeremia, Yahazieli, Yohanani, Yozabadi, Mgederathi,
5
Eluzai, Yeremothi, Bealia, Shemaria, Shefatia, Mharufi;
6
Elikana, Ishia, Azareli, Yoezeri na Yashobeamu, wana wa Kora;
7
Yoela na Zebadia, wana wa Yerohamu, kutoka Gedori.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options