Rukia maudhui

Zaburi99

Bwana Anatawala kwa Utakatifu

1
Bwana anatawala, mataifa na yatetemeke; anakalia kiti cha enzi katikati ya makerubi, dunia na itikisike.
2
Bwana ni mkuu katika Sayuni; ametukuzwa juu ya mataifa yote.
3
Wanalisifu jina lako ambalo ni kuu na la kuogopwa: yeye ni mtakatifu!

Mfalme Apendaye Haki

4
Mfalme ni mwenye nguvu na hupenda haki, wewe umethibitisha adili; katika Yakobo umefanya yaliyo haki na sawa.
5
Mtukuzeni Bwana Mungu wetu, na mkaabudu katika mahali pa kuwekea miguu yake; yeye ni mtakatifu.

Mifano ya Kihistoria ya Sala na Majibu

6
Mose na Aroni walikuwa miongoni mwa makuhani wake, Samweli alikuwa miongoni mwa walioliitia jina lake; walimwita Bwana, naye aliwajibu.
7
Alizungumza nao kutoka nguzo ya wingu; walizishika sheria zake na amri alizowapa.
8
Ee Bwana, wetu, ndiwe uliyewajibu, kwa Israeli ulikuwa Mungu mwenye kusamehe, ingawa uliadhibu matendo yao mabaya.
9
Mtukuzeni Bwana Mungu wetu, mwabuduni kwenye mlima wake mtakatifu, kwa maana Bwana Mungu wetu ni mtakatifu.
Use arrow keys to navigate
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options