- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
Zaburi34
Listen to this chapter
0:00
0:00
Kujitoa kwa Sifa za Kudumu
1
Zaburi ya Daudi, alipojifanya mwendawazimu mbele ya Abimeleki, ambaye alimfukuza, naye akaondoka. Nitamtukuza Bwana nyakati zote, sifa zake zitakuwa midomoni mwangu siku zote.
2
Nafsi yangu itajisifu katika Bwana, walioonewa watasikia na wafurahi.
3
Mtukuzeni Bwana pamoja nami, naam, na tulitukuze jina lake pamoja.
Ushuhuda wa Wokovu wa Mungu
4
Nilimtafuta Bwana naye akanijibu, akaniokoa kwenye hofu zangu zote.
5
Wale wamtazamao hutiwa nuru, nyuso zao hazifunikwi na aibu kamwe.
6
Maskini huyu alimwita Bwana, naye akamsikia, akamwokoa katika taabu zake zote.
7
Malaika wa Bwana hufanya kituo akiwazunguka wale wamchao, naye huwaokoa.
Wito wa Kuonja na Kuona
8
Onjeni mwone kwamba Bwana ni mwema, heri mtu yule anayemkimbilia.
9
Mcheni Bwana enyi watakatifu wake, kwa maana wale wamchao hawapungukiwi na chochote.
10
Wana simba wenye nguvu hutindikiwa na kuona njaa, bali wale wamtafutao Bwana hawatakosa kitu chochote kilicho chema.
Njia ya Maisha Yenye Baraka
11
Njooni, watoto wangu, mnisikilize, nitawafundisha kumcha Bwana.
12
Yeyote kati yenu anayependa uzima na kutamani kuziona siku nyingi njema,
13
basi auzuie ulimi wake na mabaya, na midomo yake kutokana na kusema uongo.
14
Aache uovu, atende mema, aitafute amani na kuifuatilia.
15
Macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, na masikio yake yako makini kusikiliza kilio chao.
16
Uso wa Bwana uko kinyume na watendao maovu, ili kufuta kumbukumbu lao duniani.
17
Wenye haki hulia, naye Bwana huwasikia, huwaokoa katika taabu zao zote.
18
Bwana yu karibu na waliovunjika moyo, na huwaokoa waliopondeka roho.
Wokovu na Ukombozi
19
Mwenye haki ana mateso mengi, lakini Bwana humwokoa nayo yote,
20
huhifadhi mifupa yake yote, hata mmoja hautavunjika.
21
Ubaya utamuua mtu mwovu, nao adui za mwenye haki watahukumiwa.
22
Bwana huwakomboa watumishi wake, yeyote anayemkimbilia yeye hatahukumiwa kamwe.
Use ← → arrow keys to navigate
Settings
Reading Style
Typeface
Font Size px
Options
Study Note