Rukia maudhui

Zaburi23

BWANA, Mchungaji Wangu Anayenipatia

1
Zaburi ya Daudi. Bwana ndiye mchungaji wangu, sitapungukiwa na kitu.
2
Hunilaza katika malisho ya majani mabichi, kando ya maji matulivu huniongoza,
3
hunihuisha nafsi yangu. Huniongoza katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.

Ulinzi na Faraja Wakati wa Hatari

4
Hata kama nikipita katikati ya bonde la uvuli wa mauti, sitaogopa mabaya, kwa maana wewe upo pamoja nami; fimbo yako na mkongojo wako vyanifariji.

Mwenyeji Mkarimu na Makao ya Milele

5
Waandaa meza mbele yangu machoni pa adui zangu. Umenipaka mafuta kichwani pangu, kikombe changu kinafurika.
6
Hakika wema na upendo vitanifuata siku zote za maisha yangu, nami nitakaa nyumbani mwa Bwana milele.
Use arrow keys to navigate
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options