Rukia maudhui

Zaburi150

Mahali na Sababu ya Kumsifu Mungu

1
Msifuni Bwana. Msifuni Mungu katika patakatifu pake, msifuni katika mbingu zake kuu.
2
Msifuni kwa matendo yake makuu, msifuni kwa kadiri ya wingi wa ukuu wake.

Vyombo vya Sifa

3
Msifuni kwa mvumo wa tarumbeta, msifuni kwa kinubi na zeze,
4
msifuni kwa matari na kucheza, msifuni kwa kinanda cha nyuzi na filimbi,
5
msifuni kwa matoazi yaliayo, msifuni kwa matoazi yavumayo sana.

Sifa kwa Mungu kwa Viumbe Wote

6
Kila chenye pumzi na kimsifu Bwana. Msifuni Bwana!
Use arrow keys to navigate
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options