Skip to content

Meshelemiah

5 mistari · 7 wanafamilia

Anajulikana pia kama: Shelemiah

Mistari inayomtaja Meshelemiah

  1. Zekaria mwana wa Meshelemia alikuwa bawabu katika ingilio la Hema la Kukutania.

  2. Hii ndiyo migawanyo ya mabawabu: Kutoka kwa wana wa Kora alikuwa: Meshelemia mwana wa Kore, mmoja wa wana wa Asafu.

  3. Meshelemia alikuwa na wana wafuatao: Zekaria mzaliwa wa kwanza, Yediaeli wa pili, Zebadia wa tatu, Yathnieli wa nne,

  4. Meshelemia alikuwa na wana na jamaa zake, waliokuwa watu wenye uwezo: jumla yao watu kumi na wanane.

  5. Kura ya Lango la Mashariki ilimwangukia Shelemia. Kisha wakapiga kura kwa Zekaria mwanawe, aliyekuwa mshauri mwenye hekima, nayo kura ya Lango la Kaskazini ikamwangukia.