Rukia maudhui
Warumi 5:1-5

Amani na Mungu kwa Njia ya Imani

Warumi 5:1-5
1
Kwa hiyo, kwa kuwa tumekwisha kuhesabiwa haki kwa imani, tuna amani na Mungu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo,
2
ambaye kwa kupitia kwake tumepata kwa njia ya imani kuifikia neema hii ambayo ndani yake sasa tunasimama, nasi twafurahia katika tumaini letu la kushiriki utukufu wa Mungu.
3
Si hivyo tu, bali twafurahi pia katika mateso, kwa sababu tunajua kuwa mateso huleta saburi,
4
nayo saburi huleta uthabiti wa moyo, na uthabiti wa moyo huleta tumaini,
5
wala tumaini halitukatishi tamaa, kwa sababu Mungu amekwisha kumimina pendo lake mioyoni mwetu kwa njia ya Roho Mtakatifu ambaye ametupatia.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options