Ufunuo 2:25-29
25
Lakini shikeni sana mlicho nacho, mpaka nitakapokuja.
26
“Atakayeshinda na kutenda mapenzi yangu mpaka mwisho, nitampa mamlaka juu ya mataifa:
27
“ ‘Atawatawala kwa fimbo ya chuma, atawavunja vipande vipande kama chombo cha udongo’: kama vile mimi nilivyopokea mamlaka kutoka kwa Baba yangu.
28
Nami nitampa pia ile nyota ya asubuhi.
29
Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo Roho ayaambia makanisa.
Settings