Skip to content
Ufunuo 2:2

Ufunuo 2:2

Inaonyesha mstari 2 pamoja na muktadha unaouzunguka.
1
“Kwa malaika wa kanisa lililoko Efeso andika: “Haya ndiyo maneno ya yule aliyezishika zile nyota saba katika mkono wake wa kuume na ambaye hutembea kati ya vile vinara saba vya taa vya dhahabu.
2
Nayajua matendo yako, bidii yako na saburi yako. Najua kuwa huwezi kuvumiliana na watu waovu na ya kwamba umewajaribu wale wanaojifanya kuwa mitume na kumbe sio, nawe umewatambua kuwa ni waongo.
3
Umevumilia na kustahimili taabu kwa ajili ya Jina langu, wala hukuchoka.
4
“Lakini nina neno dhidi yako: Umeuacha upendo wako wa kwanza.
5
Kumbuka basi ni wapi ulikoangukia! Tubu na ukafanye matendo yale ya kwanza. Kama usipotubu, nitakuja kwako na kukiondoa kinara chako cha taa kutoka mahali pake.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 90 chars

Options