Zaburi 97:1-9
1
Bwana anatawala, nchi na ifurahi, visiwa vyote vishangilie.
2
Mawingu na giza nene vinamzunguka, haki na hukumu ndio msingi wa kiti chake cha enzi.
3
Moto hutangulia mbele zake na huteketeza adui zake pande zote.
4
Umeme wake wa radi humulika dunia, nchi huona na kutetemeka.
5
Milima huyeyuka kama nta mbele za Bwana, mbele za Bwana wa dunia yote.
6
Mbingu zinatangaza haki yake, na mataifa yote huona utukufu wake.
7
Wote waabuduo sanamu waaibishwa, wale wajisifiao sanamu: mwabuduni yeye, enyi miungu yote!
8
Sayuni husikia na kushangilia, vijiji vya Yuda vinafurahi kwa sababu ya hukumu zako, Ee Bwana.
9
Kwa kuwa wewe, Ee Bwana, ndiwe Uliye Juu Sana kuliko dunia yote; umetukuka sana juu ya miungu yote.
Settings