Skip to content
Zaburi 74:4-11

Zaburi 74:4-11

4
Adui zako wamenguruma pale ulipokutana nasi, wanaweka bendera zao kama alama.
5
Walifanya kama watu wanaotumia mashoka kukata kichaka cha miti.
6
Walivunjavunja milango yote iliyonakshiwa kwa mashoka na vishoka vyao.
7
Waliteketeza kabisa mahali pako patakatifu, wakayanajisi makao ya Jina lako.
8
Walisema mioyoni mwao, “Tutawaponda kabisa!” Walichoma kila mahali ambapo Mungu aliabudiwa katika nchi.
9
Hatukupewa ishara za miujiza; hakuna manabii waliobaki, hakuna yeyote kati yetu ajuaye hali hii itachukua muda gani.
10
Ee Mungu, mtesi atakudhihaki mpaka lini? Je, adui watalitukana jina lako milele?
11
Kwa nini unazuia mkono wako, mkono wako wa kuume? Uutoe kutoka makunjo ya vazi lako na uwaangamize!
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options