Skip to content
Zaburi 74:12-17

Zaburi 74:12-17

12
Lakini wewe, Ee Mungu, ni mfalme wangu tangu zamani, unaleta wokovu duniani.
13
Ni wewe uliyeigawanya bahari kwa uweza wako; ulivunja vichwa vya wanyama wakubwa wa kutisha katika maji.
14
Ni wewe uliyeponda vichwa vya Lewiathani nawe ukamtoa kama chakula kwa viumbe vya jangwani.
15
Ni wewe uliyefungua chemchemi na vijito, ulikausha mito ambayo ilikuwa ikitiririka daima.
16
Mchana ni wako, nao usiku ni wako pia, uliziweka jua na mwezi.
17
Ni wewe uliyeiweka mipaka yote ya dunia, ulifanya kiangazi na masika.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options