Skip to content
Zaburi 74:3-9

Zaburi 74:3-9

3
Geuza hatua zako kuelekea magofu haya ya kudumu, uharibifu wote huu ambao adui ameuleta pale patakatifu.
4
Adui zako wamenguruma pale ulipokutana nasi, wanaweka bendera zao kama alama.
5
Walifanya kama watu wanaotumia mashoka kukata kichaka cha miti.
6
Walivunjavunja milango yote iliyonakshiwa kwa mashoka na vishoka vyao.
7
Waliteketeza kabisa mahali pako patakatifu, wakayanajisi makao ya Jina lako.
8
Walisema mioyoni mwao, “Tutawaponda kabisa!” Walichoma kila mahali ambapo Mungu aliabudiwa katika nchi.
9
Hatukupewa ishara za miujiza; hakuna manabii waliobaki, hakuna yeyote kati yetu ajuaye hali hii itachukua muda gani.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options