Zaburi 73:16-20
16
Nilipojaribu kuelewa haya yote, yalikuwa magumu kwangu kuelewa.
17
Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.
18
Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.
19
Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!
20
Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.
Settings