Zaburi 72:1-7
1
Zaburi ya Solomoni. Ee Mungu, mjalie mfalme aamue kwa haki yako, mwana wa mfalme kwa haki yako.
2
Atawaamua watu wako kwa haki, watu wako walioonewa kwa haki.
3
Milima italeta mafanikio kwa watu, vilima tunda la haki.
4
Atawatetea walioonewa miongoni mwa watu na atawaokoa watoto wa wahitaji, ataponda mdhalimu.
5
Atadumu kama jua lidumuvyo, kama mwezi, vizazi vyote.
6
Atakuwa kama mvua inyeshayo juu ya shamba lililofyekwa, kama manyunyu yanyeshayo ardhi.
7
Katika siku zake wenye haki watastawi; mafanikio yatakuwepo mpaka mwezi utakapokoma.
Settings