Skip to content
Zaburi 70:1

Sala ya Haraka ya Kuokolewa

Zaburi 70:1
Inaonyesha mstari 1 pamoja na muktadha unaouzunguka.
1
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Maombi. Ee Mungu, ufanye haraka kuniokoa; Ee Bwana, njoo hima unisaidie.
2
Wale wanaotafuta kuuondoa uhai wangu, waaibishwe na kufadhaishwa; wote wanaotamani kuangamizwa kwangu, warudishwe nyuma kwa aibu.
3
Wale waniambiao, “Aha! Aha!” warudi nyuma kwa sababu ya aibu yao.
4
Lakini wote wakutafutao washangilie na kukufurahia, wale wapendao wokovu wako siku zote waseme, “Mungu na atukuzwe!”
Settings

Reading style

Typeface

Font size 19px

Reading width 90 chars

Options