Skip to content
Zaburi 65:6-13

Zaburi 65:6-13

6
uliyeumba milima kwa uwezo wako, ukiwa umejivika nguvu,
7
uliyenyamazisha dhoruba za bahari, ngurumo za mawimbi yake, na ghasia za mataifa.
8
Wale wanaoishi mbali sana wanaogopa maajabu yako, kule asubuhi ipambazukiapo na kule jioni inakofifilia umeziita nyimbo za furaha.
9
Waitunza nchi na kuinyeshea, waitajirisha kwa wingi. Vijito vya Mungu vimejaa maji ili kuwapa watu nafaka, kwa maana wewe umeviamuru.
10
Umeilowesha mifereji yake na kusawazisha kingo zake; umeilainisha kwa manyunyu na kuibariki mimea yake.
11
Umeuvika mwaka taji ya baraka, magari yako yanafurika kwa wingi.
12
Mbuga za majani za jangwani umezineemesha; vilima vimevikwa furaha.
13
Penye nyanda za malisho pamejaa makundi ya wanyama, na mabonde yamepambwa kwa mavuno; vyote vinashangilia kwa furaha na kuimba.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options