Zaburi 63:1-3
1
Zaburi ya Daudi. Wakati alipokuwa katika Jangwa la Yuda. Ee Mungu, wewe ni Mungu wangu, nakutafuta kwa moyo wote; nafsi yangu inakuonea kiu, mwili wangu unakuonea wewe shauku, katika nchi kame na iliyochoka mahali ambapo hapana maji.
2
Nimekuona katika mahali patakatifu na kuuona uwezo wako na utukufu wako.
3
Kwa sababu upendo wako ni bora kuliko uhai, midomo yangu itakuadhimisha.
Settings