Zaburi 56:9-11
9
Ndipo adui zangu watarudi nyuma ninapoita msaada. Kwa hili nitajua kwamba Mungu yuko upande wangu.
10
Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Bwana, ambaye neno lake ninalisifu,
11
katika Mungu ninatumaini, sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunitenda nini?