Zaburi 51:10-13
10
Ee Mungu, uniumbie moyo safi, uifanye upya roho ya uthabiti ndani yangu.
11
Usinitupe kutoka mbele zako wala kuniondolea Roho wako Mtakatifu.
12
Unirudishie tena furaha ya wokovu wako, unipe roho ya utii, ili initegemeze.
13
Ndipo nitakapowafundisha wakosaji njia zako, na wenye dhambi watakugeukia wewe.
Settings