Zaburi 49:16-20
16
Usitishwe mtu anapotajirika, fahari ya nyumba yake inapoongezeka,
17
kwa maana hatachukua chochote atakapokufa, fahari yake haitashuka pamoja naye.
18
Ingawa alipokuwa akiishi alijihesabu kuwa heri, na wanadamu wanakusifu unapofanikiwa,
19
atajiunga na kizazi cha baba zake, ambao hawataona kamwe nuru ya uzima.
20
Mwanadamu mwenye utajiri bila ufahamu ni kama wanyama waangamiao.
Settings