Skip to content
Zaburi 38:2-8

Zaburi 38:2-8

2
Kwa kuwa mishale yako imenichoma, na mkono wako umenishukia.
3
Hakuna afya mwilini mwangu kwa sababu ya ghadhabu yako, mifupa yangu haina uzima kwa sababu ya dhambi zangu.
4
Maovu yangu yamenifunika kama mzigo usiochukulika.
5
Majeraha yangu yameoza na yananuka, kwa sababu ya upumbavu wa dhambi zangu.
6
Nimeinamishwa chini na kushushwa sana, mchana kutwa nazunguka nikiomboleza.
7
Viuno vyangu vimejaa maumivu yaunguzayo, hakuna afya mwilini mwangu.
8
Nimedhoofika na kupondwa kabisa, nasononeka kwa maumivu makuu ya moyoni.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options