Zaburi 34:17-22
17
Wenye haki hulia, naye Bwana huwasikia, huwaokoa katika taabu zao zote.
18
Bwana yu karibu na waliovunjika moyo, na huwaokoa waliopondeka roho.
19
Mwenye haki ana mateso mengi, lakini Bwana humwokoa nayo yote,
20
huhifadhi mifupa yake yote, hata mmoja hautavunjika.
21
Ubaya utamuua mtu mwovu, nao adui za mwenye haki watahukumiwa.
22
Bwana huwakomboa watumishi wake, yeyote anayemkimbilia yeye hatahukumiwa kamwe.
Settings