Skip to content
Zaburi 34:1-7

Zaburi 34:1-7

1
Zaburi ya Daudi, alipojifanya mwendawazimu mbele ya Abimeleki, ambaye alimfukuza, naye akaondoka. Nitamtukuza Bwana nyakati zote, sifa zake zitakuwa midomoni mwangu siku zote.
2
Nafsi yangu itajisifu katika Bwana, walioonewa watasikia na wafurahi.
3
Mtukuzeni Bwana pamoja nami, naam, na tulitukuze jina lake pamoja.
4
Nilimtafuta Bwana naye akanijibu, akaniokoa kwenye hofu zangu zote.
5
Wale wamtazamao hutiwa nuru, nyuso zao hazifunikwi na aibu kamwe.
6
Maskini huyu alimwita Bwana, naye akamsikia, akamwokoa katika taabu zake zote.
7
Malaika wa Bwana hufanya kituo akiwazunguka wale wamchao, naye huwaokoa.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options