Skip to content
Zaburi 31:1-8

Zaburi 31:1-8

1
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, nimekukimbilia wewe, usiache nikaaibika kamwe, kwa haki yako uniokoe.
2
Nitegee sikio lako, uje uniokoe haraka; uwe kwangu mwamba wa kimbilio, ngome imara ya kuniokoa.
3
Kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu, uniongoze na kunilinda kwa ajili ya jina lako.
4
Uniepushe na mtego niliotegewa, maana wewe ndiwe kimbilio langu.
5
Ninaikabidhi roho yangu mikononi mwako, unikomboe Ee Bwana, uliye Mungu wa kweli.
6
Ninawachukia wale wanaongʼangʼania sanamu batili; mimi ninamtumaini Bwana.
7
Nitafurahia na kushangilia upendo wako, kwa kuwa uliona mateso yangu na ulijua maumivu ya nafsi yangu.
8
Hukunikabidhi kwa adui yangu bali umeiweka miguu yangu mahali penye nafasi.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options