Zaburi 27:7-14
7
Isikie sauti yangu nikuitapo, Ee Bwana, unihurumie na unijibu.
8
Moyo wangu unasema kuhusu wewe, “Utafute uso wake!” Uso wako, Bwana “Nitautafuta.”
9
Usinifiche uso wako, usimkatae mtumishi wako kwa hasira; wewe umekuwa msaada wangu. Usinikatae wala usiniache, Ee Mungu Mwokozi wangu.
10
Hata kama baba yangu na mama wakiniacha, Bwana atanipokea.
11
Nifundishe njia yako, Ee Bwana, niongoze katika njia iliyonyooka kwa sababu ya watesi wangu.
12
Usiniachilie kwa nia za adui zangu, kwa maana mashahidi wa uongo wameinuka dhidi yangu, wakipumua ujeuri.
13
Nami bado nina tumaini hili: nitauona wema wa Bwana katika nchi ya walio hai.
14
Mngojee Bwana, uwe hodari na mwenye moyo mkuu, nawe, umngojee Bwana.
Settings