Rukia maudhui
Zaburi 25:1-7

Maombi ya Uongozi na Ulinzi

Zaburi 25:1-7
1
Zaburi ya Daudi. Kwako wewe, Ee Bwana, nainua nafsi yangu,
2
ni wewe ninayekutumainia, Ee Mungu wangu. Usiniache niaibike, wala usiache adui zangu wakanishinda.
3
Kamwe hakuna hata mmoja anayekutegemea atakayeaibishwa, bali wataaibishwa wafanyao hila bila sababu.
4
Nionyeshe njia zako, Ee Bwana, nifundishe mapito yako,
5
niongoze katika kweli yako na kunifundisha, kwa maana wewe ni Mungu Mwokozi wangu, nalo tumaini langu liko kwako wakati wote.
6
Kumbuka, Ee Bwana, rehema zako kuu na upendo, kwa maana zimekuwepo tangu zamani.
7
Usizikumbuke dhambi za ujana wangu wala njia zangu za uasi, sawasawa na upendo wako unikumbuke, kwa maana wewe ni mwema, Ee Bwana.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options