Zaburi 22:16-21
16
Mbwa wamenizunguka, kundi la watu waovu limenizingira, wametoboa mikono yangu na miguu yangu.
17
Naweza kuhesabu mifupa yangu yote, watu wananikodolea macho na kunisimanga.
18
Wanagawana nguo zangu wao kwa wao, na vazi langu wanalipigia kura.
19
Lakini wewe, Ee Bwana, usiwe mbali. Ee Nguvu yangu, uje haraka unisaidie.
20
Okoa maisha yangu na upanga, uhai wangu wa thamani kutoka nguvu za mbwa.
21
Niokoe kutoka kinywani mwa simba, niokoe kutoka pembe za mafahali mwitu.
Settings