Zaburi 21:8-12
8
Mkono wako utawashika adui zako wote, mkono wako wa kuume utawakamata adui zako.
9
Wakati utakapojitokeza utawafanya kama tanuru ya moto. Katika ghadhabu yake Bwana atawameza, moto wake utawateketeza.
10
Utawaangamiza wazao wao kutoka duniani, uzao wao kutoka wanadamu.
11
Ingawa watapanga mabaya dhidi yako na kutunga hila, hawawezi kufanikiwa,
12
kwa kuwa utawafanya wakimbie utakapowalenga usoni pao kwa mshale kutoka kwenye upinde wako.
Settings