Skip to content
Zaburi 2:1-8

Zaburi 2:1-8

1
Kwa nini mataifa wanashauriana kufanya mabaya, na kabila za watu kula njama bure?
2
Wafalme wa dunia wanajipanga na watawala wanajikusanya pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.
3
Wanasema, “Tuvunje minyororo yao na kuvitupilia mbali vifungo vyao.”
4
Yeye atawalaye mbinguni hucheka, Bwana huwadharau.
5
Kisha huwakemea katika hasira yake na kuwaogopesha katika ghadhabu yake, akisema,
6
“Nimemtawaza Mfalme wangu juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
7
Nitatangaza amri ya Bwana: Yeye aliniambia, “Wewe ni Mwanangu, leo mimi nimekuzaa.
8
Niombe, nami nitayafanya mataifa kuwa urithi wako, miisho ya dunia kuwa milki yako.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options