Skip to content
Zaburi 19:1-6

Zaburi 19:1-6

1
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Mbingu zinatangaza utukufu wa Mungu, anga zahubiri kazi ya mikono yake.
2
Siku baada ya siku zinatoa habari, usiku baada ya usiku zinatangaza maarifa.
3
Hakuna msemo wala lugha, ambapo sauti zao hazisikiki.
4
Sauti yao imeenea duniani pote, nayo maneno yao yameenea hadi miisho ya ulimwengu. Katika mbingu amepiga hema kwa ajili ya jua,
5
linafanana na bwana arusi akitoka chumbani mwake, kama shujaa afurahiavyo kukamilisha kushindana kwake.
6
Huchomoza upande mmoja wa mbingu, na kufanya mzunguko wake hadi upande mwingine. Hakuna kilichojificha joto lake.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options