Zaburi 18:16-19
16
Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
17
Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
18
Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
19
Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
Settings