Zaburi 146:7-9
7
Naye huwapatia haki walioonewa na kuwapa wenye njaa chakula. Bwana huwaweka wafungwa huru,
8
Bwana huwafumbua vipofu macho, Bwana huwainua waliolemewa na mizigo yao, Bwana huwapenda wenye haki.
9
Bwana huwalinda wageni na kuwategemeza yatima na wajane, lakini hupinga njia za waovu.