Skip to content
Zaburi 145:8-13

Zaburi 145:8-13

8
Bwana ni mwenye neema na mwingi wa huruma, si mwepesi wa hasira, bali ni mwingi wa upendo.
9
Bwana ni mwema kwa wote, ana huruma kwa vyote alivyovifanya.
10
Ee Bwana, vyote ulivyovifanya vitakusifu, watakatifu wako watakutukuza.
11
Watasimulia utukufu wa ufalme wako na kusema juu ya ukuu wako,
12
ili watu wote wajue matendo yako makuu na utukufu wa fahari ya ufalme wako.
13
Ufalme wako ni ufalme wa milele, mamlaka yako hudumu vizazi vyote. Bwana ni mwaminifu kwa ahadi zake zote na mwenye upendo kwa vyote alivyovifanya.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options