Zaburi 145:14-20
14
Bwana huwategemeza wote waangukao, na huwainua wote waliolemewa na mizigo yao.
15
Macho yao wote yanakutazama wewe, nawe huwapa chakula chao wakati wake.
16
Waufumbua mkono wako, watosheleza haja ya kila kitu kilicho hai.
17
Bwana ni mwenye haki katika njia zake zote, na mwenye upendo kwa vyote alivyovifanya.
18
Bwana yu karibu na wote wamwitao, karibu na wote wamwitao kwa uaminifu.
19
Huwatimizia wamchao matakwa yao, husikia kilio chao na kuwaokoa.
20
Bwana huwalinda wote wampendao, bali waovu wote atawaangamiza.
Settings