Zaburi 139:1-5
1
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, umenichunguza na kunijua.
2
Unajua ninapoketi na ninapoinuka; unatambua mawazo yangu tokea mbali.
3
Unafahamu kutoka kwangu na kulala kwangu; unaelewa njia zangu zote.
4
Kabla neno halijafika katika ulimi wangu, wewe walijua kikamilifu, Ee Bwana.
5
Umenizunguka nyuma na mbele; umeweka mkono wako juu yangu.
Settings