Gå til innhold
Zaburi 139:1-6

Mungu Anajua Yote

Zaburi 139:1-6
1
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, umenichunguza na kunijua.
2
Unajua ninapoketi na ninapoinuka; unatambua mawazo yangu tokea mbali.
3
Unafahamu kutoka kwangu na kulala kwangu; unaelewa njia zangu zote.
4
Kabla neno halijafika katika ulimi wangu, wewe walijua kikamilifu, Ee Bwana.
5
Umenizunguka nyuma na mbele; umeweka mkono wako juu yangu.
6
Maarifa haya ni ya ajabu mno kwangu, ni ya juu sana kwangu kuyafikia.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options