Zaburi 135:8-12
8
Alimuua mzaliwa wa kwanza wa Misri, mzaliwa wa kwanza wa wanadamu na wanyama.
9
Alipeleka ishara zake na maajabu katikati yako, ee Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
10
Aliyapiga mataifa mengi, na akaua wafalme wenye nguvu:
11
Mfalme Sihoni na Waamori, Ogu mfalme wa Bashani na wafalme wote wa Kanaani:
12
akatoa nchi yao kuwa urithi, urithi kwa watu wake Israeli.
Settings