Zaburi 121:1-4
1
Wimbo wa kwenda juu. Nayainua macho yangu nitazame vilima, msaada wangu utatoka wapi?
2
Msaada wangu hutoka kwa Bwana, Muumba wa mbingu na dunia.
3
Hatauacha mguu wako uteleze, yeye akulindaye hatasinzia,
4
hakika, yeye alindaye Israeli hatasinzia wala hatalala usingizi.