Zaburi121
Listen to this chapter
0:00
0:00
Msafiri Aangalia Juu
1
Wimbo wa kwenda juu. Nayainua macho yangu nitazame vilima, msaada wangu utatoka wapi?
2
Msaada wangu hutoka kwa Bwana, Muumba wa mbingu na dunia.
Mlinzi Asiyesinzia
3
Hatauacha mguu wako uteleze, yeye akulindaye hatasinzia,
4
hakika, yeye alindaye Israeli hatasinzia wala hatalala usingizi.
5
Bwana anakulinda, Bwana ni uvuli wako mkono wako wa kuume,
6
jua halitakudhuru mchana, wala mwezi wakati wa usiku.
Ulinzi wa Milele na Kamili
7
Bwana atakukinga na madhara yote, atayalinda maisha yako,
8
Bwana atakulinda unapoingia na unapotoka, tangu sasa na hata milele.
Use ← → arrow keys to navigate
Settings
Reading Style
Typeface
Font Size px
Reading Width chars
Options
Study Note