Zaburi 119:41-45
41
Ee Bwana, upendo wako usiokoma unijie, wokovu wako sawasawa na ahadi yako,
42
ndipo nitakapomjibu anayenidhihaki, kwa kuwa ninalitumainia neno lako.
43
Usilinyakue neno la kweli kutoka kinywani mwangu, kwa kuwa nimeweka tumaini langu katika amri zako.
44
Nitaitii amri yako daima, naam, milele na milele.
45
Nitatembea nikiwa huru, kwa kuwa nimejifunza mausia yako.
Settings