Zaburi 119:115-117
115
Ondokeni kwangu, ninyi mtendao mabaya, ili niweze kushika amri za Mungu wangu!
116
Nihifadhi sawasawa na ahadi yako, nami nitaishi; usiache matumaini yangu yakavunjwa.
117
Nitegemeze, nami nitaokolewa, nami daima nitayaheshimu maagizo yako.