Zaburi 112:6-9
6
Hakika hatatikisika kamwe, mtu mwenye haki atakumbukwa milele.
7
Hataogopa habari mbaya, moyo wake ni thabiti, ukimtegemea Bwana.
8
Moyo wake ni salama, hatakuwa na hofu, mwishoni ataona ushindi dhidi ya adui zake.
9
Ametawanya vipawa vyake kwa ukarimu akawapa maskini; haki yake hudumu milele; pembe yake itatukuzwa kwa heshima.
Settings