Zaburi 111:4-9
4
Amefanya maajabu yake yakumbukwe, Bwana ni mwenye neema na huruma.
5
Huwapa chakula wale wanaomcha, hulikumbuka agano lake milele.
6
Amewaonyesha watu wake uwezo wa kazi zake, akiwapa nchi za mataifa mengine.
7
Kazi za mikono yake ni za uaminifu na haki, mausia yake yote ni ya kuaminika.
8
Zinadumu milele na milele, zikifanyika kwa uaminifu na unyofu.
9
Aliwapa watu wake ukombozi, aliamuru agano lake milele: jina lake ni takatifu na la kuogopwa.
Settings