Zaburi 107:5-9
5
Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
6
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
7
Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
8
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
9
kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
Settings