Skip to content
Zaburi 107:10-16

Zaburi 107:10-16

10
Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
11
kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
12
Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
13
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
14
Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
15
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
16
kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options