Zaburi 105:8-11
8
Hulikumbuka agano lake milele, neno ambalo aliamuru, kwa vizazi elfu,
9
agano alilolifanya na Abrahamu, kiapo alichomwapia Isaki.
10
Alilithibitisha kwa Yakobo kuwa amri, kwa Israeli liwe agano la milele:
11
“Nitakupa wewe nchi ya Kanaani kuwa sehemu utakayoirithi.”