Zaburi 105:7-15
7
Yeye ndiye Bwana Mungu wetu, hukumu zake zimo duniani pote.
8
Hulikumbuka agano lake milele, neno ambalo aliamuru, kwa vizazi elfu,
9
agano alilolifanya na Abrahamu, kiapo alichomwapia Isaki.
10
Alilithibitisha kwa Yakobo kuwa amri, kwa Israeli liwe agano la milele:
11
“Nitakupa wewe nchi ya Kanaani kuwa sehemu utakayoirithi.”
12
Walipokuwa wachache kwa idadi, wachache sana na wageni ndani yake,
13
walitangatanga kutoka taifa moja hadi jingine, kutoka ufalme mmoja hadi mwingine.
14
Hakuruhusu mtu yeyote awaonee; kwa ajili yao aliwakemea wafalme, akisema:
15
“Msiwaguse niliowatia mafuta; msiwadhuru manabii wangu.”
Settings