Zaburi 105:43-45
43
Aliwatoa watu wake kwa furaha, wateule wake kwa kelele za shangwe,
44
akawapa nchi za mataifa, wakawa warithi wa mali wengine walikuwa wameitaabikia:
45
alifanya haya ili wayashike mausia yake na kuzitii sheria zake. Msifuni Bwana.